Waasi wa M23 wawauwa walinda amani 9 wa Afrika Kusini
26 Januari 2025Taarifa ya wizara hiyo imefafanua kuwa, walinda amani saba kati ya waliouwawa kufikia Ijumaa walikuwa sehemu ya jeshi la Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika SADC, wakati wengine wawili walikuwa kutoka Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Kongo MONUSCO.
Nalo jeshi la Uruguay lilitangaza kuwa, mwanajeshi wake mmoja aliyekuwa sehemu ya Ujumbe wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo ameuwawa na wanajeshi wengine watano wamejeruhiwa.
Soma zaidi: Guterres ahofia kuongezeka kwa mzozo wa DRC
Takriban walinda amani 15,000 wa Umoja wa Mataifa wako nchini Kongo wakati kukiwa na mapambano makali mashariki mwa Kongo kati ya jeshi la nchi hiyo dhidi ya waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda.
Hayo yanajiri wakati Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa likitarajiwa kufanya kikao cha dharura leo Jumapili kuhusu hali nchini humo baada ya Kinshasa kuwaondoa wanadiplomasia wake nchini Rwanda wakati waasi wa M23 wakiendelea kusonga mbele Goma.