Wakaguzi wa IAEA waondoka Tehran
4 Julai 2025Matangazo
Kupitia ukurasa wa X, shirika hilo limeeleza kuwa Mkurugenzi wake Rafael Grossi amesisitiza umuhimu mkubwa wa IAEAkuendelea na majukumu yake ya kufuatilia nyuklia Iran haraka iwezekanavyo.
Kusitishwa kwa shughuli za shirika hilo kulitangazwa baada ya kumalizika kwa vita vya siku 12 vya Israel na Iran vilivyotokea mwezi uliopita ambapo Marekani na Israel zilivishambulia vituo vya nyuklia vya Tehran.
Juni 25 siku moja baada ya mapigano kusimamishwa kati ya nchi hizo mbili, wabunge wa Iran, kwa sauti moja walipiga kura kusitisha shughuli za shirika hilo nchini humo.