MigogoroMashariki ya Kati
Wapalestina 51 wauwawa wakisubiri malori ya misaada Gaza
17 Juni 2025Matangazo
Wizara ya afya ya ukanda huo imebainisha kuwa makumi ya watu wamejeruhiwa. Wizara hiyo imeongeza kuwa hospitali ya Nasser ambako majeruhi wamepelekwa kwa matibabu imeelemewa na idadi ya vifo na watu waliojeruhiwa wakati wakiyasubiri malori ya Umoja wa mataifa yaliyobeba msaada wa chakula.
Soma zaidi: Israel yaendelea kushambulia maeneo ya misaada Gaza
Kiwango cha vifo kinatazamiwa kuongezeka kwakuwa wengi wa majeruhi wako katika hali mbaya. Jeshi la Israel halijatoa tamko lolote kuhusu shambulio hilo.