MigogoroMashariki ya Kati
Mashambulizi ya Israel yawauwa wakaazi 29 Gaza
2 Mei 2025Matangazo
Watu hao wameuawa katika mashambulizi tofauti yakiwemo yaliyoyalenga maeneo ya Bureij katikati mwa Gaza, Bet Lahiya, na sehemu nyingine za ukanda huo.
Soma zaidi: Wapalestina 52,400 wameuawa ndani ya miezi 18 iliyopita Gaza
Hayo yanajiri wakati Shirika la Kimataifa la Msalaba Mwekundu likionya kuwa huduma za kiutu katika Ukanda wa Gaza zinaelekea kuporomoka kabisa baada ya Israel kuzuia misaada kuingia kwenye eneo hilo lililoathiriwa na vita.
Shirika hilo limesema bila ya misaada kuanza haraka kuingizwa Gaza, litashindwa kupata chakula, dawa na vifaa vingine vya kuokoa maisha vinavyohitajika ili kuendeleza shughuli zake.