Wahamiaji 500 waokolewa Ugiriki
26 Mei 2025Matangazo
Miongoni mwa waliookolewa ni wahamiaji 280 katika misafara mitano tafauti, ambao ndani yake walikuwamo watoto 13, kwa mujibu wa walinzi wa pwani wa Ugiriki.
Kisiwa cha Crete kinachotazamana na Libya na Misri kimekuwa kikipokea idadi kubwa ya wahamiaji katika miaka ya hivi karibuni.
Soma zaidi: Wahamiaji wahamishwa kambi ya Idomeni
Wahamiaji hao hutumia njia za hatari na mashua zisizo salama kuvuukia, ambapo miaka miwili iliyopita meli iliyosheheni watu kwenye ujia wa kusini magharibi wa Peloponnese ilizama na kuuwa watu zaidi ya 600 waliokuwamo, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.