Utawala wa sheriaAfrika
Kongo: Wafungwa 375 watoroka kutoka gerezani Tanganyika
20 Februari 2025Matangazo
Wafungwa hao walitoroka katika gereza la Tanganyika wakati walipokuwa wakijiandaa kuingizwa kwenye vyumba vyao ambapo baadhi walisikika wakilalamika kuwa waasi wa M23 wamewasili mjini Kalemie, swala lililozua tafrani katika gereza hilo.
Wafungwa hao walitoroka kwa kuruka ukuta kabla ya lango kuu kufunguliwa. Askari magereza walifyetuwa risasi takribani dakika 20, na baadhi ya wafungwa wakasalia gerezani.
Soma pia:Wafungwa 6,000 watoroka gereza lenye ulinzi mkali Msumbiji katika vurugu za uchaguzi
Taarifa zinasema wafungwa 379 kati ya wafungwa 658 wametoroka. Raia wa jimbo la Tanganyika wanaishi kwa wasiwasi kutokana na kadhia hiyo pamoja na milio ya risasi.