MigogoroAfrika
Mzozo wa Kongo wasababishaa hofu kwa wafanyabiashara Rwanda
10 Machi 2025Matangazo
Madereva wa malori hayo ya mizigo wanayoichukua katika bandari ya Dar es Salaam, Tanzania wanaeleza kwamba wanakumbana na mashambulizi ya watu ambao ni raia wa Kongo na ambao wana hasira kwamba Rwanda inawaunga mkono wapiganaji wa M23.
Jamhuri ya Kideomkrasia ya Kongo ni mshirika wa pili kwa ukubwa wa kibiashara wa Rwanda, ikinunua bidhaa zenye thamani ya dola milioni 156 katika miezi tisa ya kwanza ya 2024, kulingana na Taasisi ya Kitaifa ya Takwimu.
Soma pia:Mashambulizi ya ADF yasababisha mauaji ya watu 9 Kongo
Wasafirishaji wa mizigo wa Rwanda sasa wana hofu kwamba mzozo unaoendelea mashariki mwa Kongo utaendelea kuziathiri biashara zao za usafirishaji.