SiasaChina
Brazil yaishitaki kampuni ya magari ya Kichina kwa utumwa
28 Mei 2025Matangazo
Ofisi ya mwendesha mashitaka ya jimbo la Bahia imesema kwenye taarifa yake kwamba inaiomba mahakama kutowa fidia ya dola milioni 50 za Kimarekani kwa madhara yaliyosababishwa na kampuni hiyo ya Kichina.
Mashitaka hayo yanatokana na uchunguzi uliofanyika mwaka jana na kupelekea kuokolewa kwa wafanyakazi 220 wa Kichina kwenye kiwanda kipya cha kampuni ya BYD katika mji wa Camacari.
Soma zaidi: Mataifa yanayoendelea yakabiliwa na wimbi baya la madeni ya China - Ripoti
Waendesha mashitaka wanasema wafanyakazi hao waliingizwa nchini Brazil kwa nyaraka na vibali vya uongo.
Msemaji wa kampuni hiyo ameyaita madai hayo kuwa ya uongo na yenye lengo la kuidhalilisha China na bidhaa zake.