Waasi wa M23 nchini waondoka katika mji wa Walikale
4 Aprili 2025Matangazo
Kwa mujibu wa vyanzo kutoka pande zote zinazohasimiana vimesema kwamba serikali ya Kongo na waasi wa M23 wanapanga kukutana nmjini Doha nchini Qatar mnamo Aprili 9.
Soma pia:Kongo na waasi wa M23 kuanza mazungumzo ya ana kwa ana
Akithibitisha kuondoka kwa M23, msemaji wa jeshi la Kongo Sylvain Ekenge siku ya Ijumaa alisema kwamba wanajeshi wake wameshuhudia kuondoa kwao.
Waasi wa M23 waliahidi kujiondoa Walikale mwezi uliopita ila hawakufanya hilo baada ya kuwashutumu wanajeshi wa Kongo kwa kukiuka ahadi ya kujiondoa na kusitisha mashambulizi ya ndege zisizo na rubani.