Vyombo vya habari vya Iran vyaripoti mlipuko mjini Tehran
15 Juni 2025Matangazo
Shirika la habari la Tasnim, lilichapisha video ya eneo la mkasa na kusema ulitokea karibu na eneo la kati la Valiasr.
Video hiyo, pia ilionyesha moshi ukifuka kutoka eneo hilo la tukio, huku vifusi na vioo vilivyopasuka vikiwa vimetawanyika. Vyombo vingine vya habari pia viliripoti taarifa sawa na hiyo.
Askari 7 wa Israel wajeruhiwa, huku wanasayansi watatu wa Iran wakiuawa
Katika hatua nyingine, Iran imesema kuwa haikutuma ujumbe wowote kwa Israel kupitia nchi ya tatu. Haya yamesemwa leo na msemaji wa wizara ya mambo ya nje Esmail Baghaei baada ya Rais wa Cyprus Nikos Christodoulides kusema mapema kwamba Iran iliiomba nchi yake kuwasilisha baadhi ya ujumbe kwaIsraeli.