Vurugu zashuhudiwa Vatican watu wakiendelea kumuaga Papa
25 Aprili 2025Matangazo
Shirika la habari la dpa, limeripoti kuwa watu wanaopanga foleni kwenye barabara ya Via della Conciliazione, njia kuu ya kufikia uwanja wa Matakatifu Petero, walisukuma kando vizuizi vya usalama na kulazimisha kuingia katika kanisa hilo huku maafisa wa usalama wakijaribu kuwazuia.
Maelfu wanaendelea kumuaga Papa Francis leo
Mwili wa Papa Francis unatarajiwa kuwa katika kanisa hilo hadi saa moja jioni leo kwa majira ya Vaticankabla ya jeneza lake kufungwa kwa ibada ya mazishi na kuzikwa hapo kesho.
Wakristo kote duniani wamuombea Papa Francis
Vatican imesema takriban ujumbe 130 wa kigeni umethibitisha kuhudhuria mazishi hayo ya Papa ikiwa ni pamoja na wakuu 50 wa mataifa na wafalme 10.