Vita vya mpaka kati ya Thailand na Cambodia vyatanuka
25 Julai 2025Takribani watu 20 wamepoteza maisha na zaidi ya watu 130,000 kulazimika kukimbia makazi yao, katika kile kinachotajwa kuwa ghasia mbaya zaidi kati ya majirani hao wa Asia ya Kusini-Mashariki katika kipindi cha miaka 13.
Wakati Waziri Mkuu wa Cambodia Hun Manet akisema Thailand ilikubali pendekezo la kusitisha mapigano lililotolewa na Waziri Mkuu wa Malaysia Anwar Ibrahim kabla ya kulibatilisha, serikali ya Thailand haijatoa tamko rasmi.
Zaidi ya watu laki moja watoroka eneo la mpakani la Thailand na Cambodia
Mapigano hayo yameenea kutoka maeneo sita hadi zaidi ya 12, huku Thailand ikiilaumu Cambodia kwa kushambulia raia kwa kutumia makombora ya Urusi aina ya BM-21, na kuitaja hatua hiyo kuwa ni uhalifu wa kivita.
Kwa upande mwingine, Cambodia imelitaka Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuingilia kati, ikizingatiwa kuwa haina ndege za kivita wala vifaa vya kijeshi vya kisasa ikilinganishwa na Thailand.